Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 133. Mamlaka ya Huruma ya Rais

(1) Kwa ombi la mtu yeyote, Rais anaweza kutekeleza mamlaka yake ya msamaha kwa mujibu wa ushauri kutoka kwa Kamati ya Ushauri iliyoundwa katika Kifungu cha (2) , kwa–

  • (a) Kumsamehe kabisa au kwa masharti mtu ambaye amepatikana na hatia;
  • (b) kuahirisha utekelezaji wa adhabu kwa muda uliowekwa au kwa muda usiojulikana;
  • (c) Kubadili adhabu isiwe kali; au
  • (d) Kusamehe sehemu ya adhabu au adhabu yote.

(2) Kutakuwepo na Kamati ya Ushauri kuhusu Mamlaka ya Msamaha wa Rais, itakayowahusisha–

  • (a) Mwanasheria Mkuu;
  • (b) Waziri anayehusika na Huduma za Urekebishaji; na
  • (c) Angalau watu wengine watano,na wasiwe watu walio kwenye huduma ya umma au afisi za Serikali kama inavyoidhinishwa na Sheria ya Bunge.

(3) Bunge litatunga Sheria ili kubainisha–

  • (a) hatamu ya wanachama wa Kamati ya Ushauri;
  • (b) Taratibu za Kamati ya Ushauri; na
  • (c) Kigezo ambacho kitatumiwa na Kamati ya Ushauri katika kuunda ushauri wake.

(4) Kamati ya Ushauri inaweza kutilia maanani maoni ya waathiriwa wa hatia kuhusu yale inayompendekezea Rais.