Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 233. Tume ya Huduma za Umma

(1) Tume imeundwa ya Huduma za Umma.

(2) Tume ya Huduma za Umma inahusisha mwenyekiti, naibu wa mwenyekiti na wanachama wengine saba walioteuliwa na Rais na kuidhinishwa na Baraza Kuu la Kitaifa.

(3) Kwa mujibu wa ibara ya (4), mtu hastahili kuteuliwa kama mwanachama wa Tume hii iwapo mtu huyo–

  • (a) kwa kipindi cha miaka mitano iliyotangulia alikuwa na afisi au amewania kiti katika uchaguzi kama–
    • (i) mwanachama wa bunge au wa baraza la kaunti; au
    • (ii) mwanachama katika bodi ya uongozi ya chama cha kisiasa;
  • (b) ana wadhifa katika afisi yoyote ya serikali;
  • (c) anagombea kiti, au kwa wakati wowote amewahi kugombea kiti cha ubunge au katika baraza la kaunti; au
  • (d) anashikilia, au kwa wakati wowote ule, amewahi kushikilia kiti cha afisi ya shirika la kisiasa linalofadhili au kuunga mkono mgombeaji wa ubunge au wa baraza la kaunti. (4) ibara ya (3) (c) na (d) hazitatumika iwapo uchaguzi mkuu umefanywa mara mbili tangu mtu huyo alipogombea kiti au alipokuwa afisini.

(5) Kutakuwa na katibu wa Tume.

(6) Katibu wa Tume–

  • (a) ndiye afisa mkuu wa Tume; na
  • (b) atateuliwa na Tume kwa kipindi cha miaka mitano na anaweza kuteuliwa upya mara moja tu.