Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

2. Kuahirisha Masharti ya Katiba Hii

(1) Masharti yafuatayo ya Katiba hii yameahirishwa mpaka matangazo ya mwisho ya majibu yote ya uchaguzi mkuu wa kwanza wa Bunge chini ya Katiba hii–

  • (a) Sura ya Saba, isipokuwa masharti ya sura hii yatahusu uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya Katiba hii;
  • (b) Sura ya Nane , isipokuwa masharti ya sura hii yanayohusiana na uchaguzi wa Baraza Kuu la Kitaifa na Seneti yatahusishwa katika uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya Katiba hii; na
  • (c) Vifungu vya 129 hadi 155 vya Sura ya Tisa, isipokuwa masharti ya Sura yanayohusiana na uchaguzi wa Rais, yatahusishwa katika uchaguzi mkuu wa kwanza chini ya Katiba hii.

(2) Masharti ya Katiba hii yanayohusu serikali ya ugatuzi, kukiwemo kifungu cha 187, yamesimamishwa hadi tarehe ya uchaguzi wa kwanza wa mabaraza ya kaunti na magavana utakaofanywa chini ya Katiba hii.

(3) Licha ya ibara ndogo ya (2)–

  • (a) Uchaguzi wa mabaraza ya kaunti na magavana utafanywa kwa mujibu wa vifungu vya 177 na 180 vya Katiba hii; na
  • (b) Sheria zinazohusu serikali ya ugatuzi, zinazohitajika katika Mpangilio huu na katika Sura za Kumi na Moja na Kumi Mbili za Katiba hii, zitatungwa katika muda uliowekwa katika Mpangilio wa Tano.

(4) Kifungu cha 62 (2) na (3) kimeahirishwa mpaka Tume ya Kitaifa ya Ardhi itakapoundwa.