Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 147. Majukumu ya Naibu wa Rais

(1) Naibu wa rais atakuwa msaidizi mkuu wa Rais na atakuwa kaimu Rais katika utekelezaji wa majukumu ya Rais.

(2) Naibu wa rais atatekeleza majukumu yaliyotunukiwa kwake na Katiba hii na majukumu mengine yoyote ya Rais anayoweza kupewa na Rais mwenyewe.

(3) Kwa kutegemea Kifungu cha 134, wakati Rais hayupo au hawezi kutekeleza majukumu yake kwa muda mfupi na katika kipindi kingine chochote ambacho Rais anaweza kuamua, Naibu wa rais atakuwa kaimu wa Rais.

(4) Naibu hatashikilia mamlaka ya afisi nyingine ya Serikali au umma.