Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 205. Mashauriano Kuhusu Sheria za Kifedha Zinazoathiri Kaunti

(1) Wakati mswada ambao unahusisha ugavi wa mapato, au suala lolote la kifedha linalohusu serikali za kaunti utakapochapishwa, Tume ya ugavi wa Mapato itachunguza mahitaji yake na kutoa mapendekezo kwa Baraza la Kitaifa na Seneti.

(2) Mapendekezo yoyote ya Tume hii yatawasiliswa Bungeni, na kila bunge litachunguza mapendekezo hayo kabla ya kupiga kura.