Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 170. Mahakama za Kadhi

(1) Kutakuwa na Kadhi Mkuu na idadi kama hiyo, isiwe chini ya watatu, ya kadhi wengine kulingana na itakavyopendekezwa chini ya Sheria ya Bunge.

(2) Mtu hatahitimu kuteuliwa kushikilia au kuhudumu katika wadhifa wa Kadhi isipokuwa mtu huyo–

  • (a) anakiri kwa dini ya Uislamu; na
  • (b) ana maarifa ya sheria ya Uislamu kama inavyokubalika na madhehebu ya Waislamu, ambayo kwa mujibu wa Tume ya Huduma za Mahakama, amehitimu kuongoza vikao vya mahakama ya Kadhi.

(3) Bunge litabuni mahakama za kadhi, na kila mahakama ya Kadhi itakuwa na mamlaka kulingana na jinsi itakavyoidhinishwa na sheria, kwa mujibu wa Ibara ya (5).

(4) Kadhi Mkuu na Kadhi wengine, au Kadhi Mkuu na Makadhi wengine kama hao (wasiopungua watatu) kama ilivyoidhinishwa na Sheria ya Bunge, watapewa uwezo kila mmoja wa kuhudumu kwa mahakama ya Kadhi iliyo na mamlaka nchini Kenya.

(5) Mamlaka ya mahakama ya Kadhi yatahusisha kubainisha maswali ya sheria ya Uislamu kuhusiana na hadhi ya kibinafsi, ndoa, talaka au urithi katika kesi ambazo pande husika zinakiri dini ya Uislamu na kutii mamlaka ya mahakama za kadhi.