Ukusanyaji wa Mapato ya Serikali za Kaunti
Mwaka wa Fedha wa 2017/2018
Lengo la jumla la mapato ya kila mwaka la kaunti katika Mwaka wa Fedha wa 2017/18 lilikuwa shilingi bilioni 49.22 ikilinganishwa na ukusanyaji halisi wa shilingi 32.49 bilioni, ambazo zilikuwa asilimia 66 ya lengo.
Huu ulikuwa upungufu kidogo ukilinganishwa na shilingi bilioni 32.52 zilizozalishwa katika Mwaka wa Fedha wa 2016/17 (ambazo zilikuwa asilimia 56.4 ya lengo la mapato ya mwaka huo).
Kaunti | Lengo la Mwaka | Mapato Halisi | Mapato Halisi/ Lengo la Mwaka (%) |
---|---|---|---|
Baringo | 350,000,000 | 301,404,377 | 86.1 |
Bomet | 200,211,165 | 181,375,343 | 90.6 |
Bungoma | 865,554,992 | 656,750,139 | 75.9 |
Busia | 412,155,210 | 176,294,585 | 42.8 |
Elgeyo/Marakwet | 160,291,113 | 105,483,195 | 65.8 |
Embu | 653,490,000 | 416,111,597 | 63.7 |
Garissa | 250,000,000 | 86,687,563 | 34.7 |
Homa Bay | 118,664,278 | 106,939,465 | 90.1 |
Isiolo | 182,861,337 | 114,557,116 | 62.6 |
Kajiado | 1,040,794,334 | 682,162,558 | 65.5 |
Kakamega | 774,571,849 | 440,611,031 | 56.9 |
Kericho | 554,641,236 | 414,048,710 | 74.7 |
Kiambu | 3,227,491,771 | 1,693,708,234 | 52.5 |
Kilifi | 929,663,257 | 523,347,190 | 56.3 |
Kirinyaga | 600,000,000 | 343,970,322 | 57.3 |
Kisii | 950,000,000 | 256,284,854 | 27.0 |
Kisumu | 1,148,685,296 | 874,901,775 | 76.2 |
Kitui | 579,158,072 | 335,122,477 | 57.9 |
Kwale | 275,000,000 | 276,295,129 | 100.5 |
Laikipia | 500,000,000 | 413,328,186 | 82.7 |
Lamu | 90,000,000 | 55,286,688 | 61.4 |
Machakos | 1,594,386,715 | 1,063,726,784 | 66.7 |
Makueni | 600,000,000 | 319,282,234 | 53.2 |
Mandera | 231,000,000 | 61,813,295 | 26.8 |
Marsabit | 130,000,000 | 83,390,480 | 64.1 |
Meru | 821,775,812 | 441,690,937 | 53.7 |
Migori | 200,000,000 | 222,251,290 | 111.1 |
Mombasa | 3,595,744,681 | 3,159,156,334 | 87.9 |
Murang’a | 850,000,000 | 453,706,818 | 53.4 |
Nairobi City | 17,229,008,928 | 10,109,419,494 | 58.7 |
Nakuru | 2,500,000,000 | 2,278,646,064 | 91.1 |
Nandi | 385,438,659 | 197,886,883 | 51.3 |
Narok | 2,483,456,238 | 2,188,436,615 | 88.1 |
Nyamira | 253,112,676 | 96,617,045 | 38.2 |
Nyandarua | 371,000,000 | 318,585,599 | 85.9 |
Nyeri | 1,000,000,000 | 760,225,951 | 76.0 |
Samburu | 301,230,000 | 257,292,957 | 85.4 |
Siaya | 270,000,000 | 139,336,798 | 51.6 |
Taita/Taveta | 398,465,509 | 193,595,795 | 48.6 |
Tana River | 30,000,000 | 56,625,198 | 188.8 |
Tharaka-Nithi | 179,915,283 | 126,606,742 | 70.4 |
Trans Nzoia | 400,000,000 | 246,062,902 | 61.5 |
Turkana | 200,000,000 | 143,896,898 | 71.9 |
Uasin Gishu | 850,000,000 | 819,220,211 | 96.4 |
Vihiga | 220,000,000 | 143,530,752 | 65.2 |
Wajir | 150,000,000 | 67,608,475 | 45.1 |
West Pokot | 111,245,626 | 88,411,177 | 79.5 |
Jumla | 49,219,014,037 | 32,491,694,261 | 66.0 |
Kutoka tarehe 1 Julai 2017 hadi 30 Juni 2018. Asili: Ripoti ya Msimamizi wa Bajeti ya 2017/18 (PDF)
Katika kipindi kinachoangaziwa, kaunti zilizopata kiwango cha juu zaidi cha mapato ya ndani zilikuwa–
- Nairobi City kwa shilingi bilioni 10.11,
- Mombasa kwa shilingi bilioni 3.16, na
- Nakuru kwa shilingi bilioni 2.28.
Kaunti zilizozalisha kiasi cha chini zaidi zilikuwa–
- Lamu kwa shilingi milioni 55.29,
- Tana River kwa shilingi milioni 56.63, na
- Mandera kwa shilingi milioni 61.82.
Uchambuzi wa mapato ya ndani kama sehemu ya lengo la mapato ya kila mwaka unaonyesha kuwa kaunti tatu zilivuka malengo yao, ambazo ni–
- Tana River kwa asilimia 188.8,
- Migori kwa asilimia 111.1, na
- Kwale kwa asilimia 100.5.
Kaunti ambazo zilirekodi kiwango cha chini zaidi cha mapato ya ndani dhidi ya malengo ya mwaka zilikuwa–
- Garissa kwa asilimia 34.7,
- Kisii kwa asilimia 27, na
- Mandera kwa asilimia 26.8.