Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 155. Makatibu Wakuu

(1) Kutabuniwa afisi ya Katibu Mkuu ambayo ni afisi katika huduma ya umma.

(2) Kila Wizara au idara ya Serikali itakuwa chini ya usimamizi wa Katibu Mkuu.

(3) Rais–

  • (a) atapendekeza mtu ili kuteuliwa kama Katibu Mkuu kutoka miongoni mwa wale waliopendekezwa na Tume ya Huduma za Umma; na
  • (b) atamteua Katibu Mkuu kwa idhini ya Baraza la Kitaifa.

(4) Rais anaweza kubadilisha au kumhamisha kazi Katibu Mkuu.

(5) Katibu Mkuu anaweza kujiuzulu kwa kumuandikia Rais notisi