Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 116. Kutekelezeka kwa Sheria

(1) Mswada unaopitishwa na Bunge na kuidhinishwa na Rais, utachapishwa katika Gazeti Rasmi la Serikali kama Sheria ya Bunge katika muda wa siku saba baada ya kuidhinishwa.

(2) Kwa kuzingatia ibara ya (3), Sheria ya Bunge inaanza kutekelezwa baada ya siku ya kumi na nne za kuchapishwa kwake katika Gazeti Rasmi la Serikali isipokuwa pale ambapo Sheria yenyewe inapendekeza tarehe au wakati wa kuanza kutekelezwa kwake.

(3) Sheria ya Bunge ambayo moja kwa moja inatunukia maslahi ya kifedha kwa wabunge, haitaidhinishwa hadi baada ya uchaguzi mkuu wa wabunge unaofuatia.

(4) ibara ya (3) haitatumika kwa maslahi walionayo wabunge wakiwa kama wananchi.