Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 111. Miswada Maalumu Inayohusu Serikali za Kaunti

(1) Mswada maalumu unaohusu serikali za kaunti utashughulikiwa kwa namna moja kama mswada wa kawaida unaohusu serikali za kaunti kuambatana na ibara ya ya (2) na (3).

(2) Baraza la Kitaifa linaweza kurekebisha au kupiga marufuku mswada maalum uliopitishwa na Seneti kwa uamuzi tu ulioungwa mkono na angalau thuluthi mbili ya wabunge.

(3) Iwapo uamuzi katika Baraza la Kitaifa wa kurekebisha au kupiga marufuku mswada maalum utaangushwa, Spika wa Bunge ataupeleka mswada kwa hali iliyokubaliwa na Seneti kwa Rais katika muda wa siku saba ili kuidhinishwa.