Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 107. Kuongoza Vikao Bungeni

(1) Katika kikao chochote cha Bunge–

  • (a) Spika ndiye kiongozi;
  • (b) Ikiwa Spika hayupo, Naibu wa Spika ataongoza; na
  • (c) Spika na Naibu wake wasipokuwepo, mbunge mwingine yeyote atakayechaguliwa na Bunge ataongoza;

(2) Katika kikao cha pamoja kati ya Mabunge, Spika wa Baraza la Kitaifa litaongoza likisaidiwa na Spika wa Seneti.