Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 103. Kuondoka Afisini kwa Mbunge

(1) Afisi ya mbunge itakuwa wazi–

  • (a) ikiwa mbunge huyo amefariki;
  • (b) ikiwa, katika kipindi cha mbunge huyo anakosekana katika vikao vinane mfululizo vya bunge husika, bila ruhusa ya Spika wa kitengo chake cha bunge kwa maandishi, na hatoi sababu ya kuridhisha ya kutohudhuria kwake kwa kamati husika;
  • (c) ikiwa kwa vinginevyo mbunge huyo ataondolewa afisini chini ya Katiba hii au sheria iliyotungwa chini ya Kifungu cha 80;
  • (d) ikiwa mbunge huyo atajiuzulu kwa kumwandikia barua Spika;
  • (e) ikiwa, ameshachaguliwa katika Bunge–
    • (i) kama mwanachama wa chama cha kisiasa, mwanachama huyu anajiuzulu kutoka kwa chama au angefaa kujiuzulu kutoka kwa chama kama inavyoamriwa kwa mujibu wa sheria inayozingatiwa na ibara ya (2); au
    • (ii) kama mgombea uchaguzi wa kibinafsi, anajiunga na chama cha kisiasa.
  • (f) baada ya kukamilika kwa muhula wa Bunge husika;
  • (g) ikiwa mbunge huyo ataondolewa katika ugombeaji wa kuchaguliwa Bungeni chini ya Kifungu cha 99 (2) (d) hadi (h).

(2) Bunge litatunga sheria ili kuruhusu hali ambazo mwanachama wa chama cha kisiasa atachukuliwa kama, kwa makusudi ya ibara ya (1) (e), aliyejiuzulu kutoka kwa chama.