Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 90. Ugawaji wa Orodha ya Viti vya Chama

(1) Uchaguzi wa viti bungeni uliotolewa chini ya Kifungu cha 97 (1) (c) na 98 (1) (b), (c) na (d), na wanachama wa baraza la kaunti chini ya kifungu cha 177 (1) (b) na (c),utakuwa kwa misingi ya ushirikishwaji sawa kwa kutumia orodha za vyama.

(2) Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka itawajibika katika kuendesha na kusimamia chaguzi za viti vilivyotolewa chini ya Ibara ya (1) na itahakikisha kwamba–

  • (a) kila chama cha kisiasa kinachoshiriki katika uchaguzi mkuu kitateua na kuwasilisha orodha ya majina ya watu wote ambao wangalichaguliwa iwapo chama hicho kingalipewa viti vyote kama ilivyo chini ya Ibara ya (1), kwa wakati ulioagizwa kupitia sheria ya kitaifa;
  • (b) isipokuwa kwenye viti vilivyoelezewa chini ya Kifungu cha cha 98 (1) (b), kila orodha ya vyama ina idadi kamilifu ya wagombeaji wanaostahili na hubadilishana kati ya wagombeaji wanaume na wanawake kulingana na jinsi walivyoorodheshwa ; na
  • (c) isipokuwa kwenye viti vya baraza la kaunti, kila orodha ya chama inaakisi tofauti za kimaeneo na uanuwai wa kikabila wa Wakenya.

(3) Viti vilivyotajwa katika ibara ya (1) vitagawiwa vyama vya kisiasa kwa kulingana na idadi ya jumla ya viti walivyoshinda wagombeaji wa chama cha kisiasa katika uchaguzi mkuu.