Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 6. Ugatuzi na Kufikia Huduma

(1) Eneo la Kenya limegawanywa katika kaunti zilizotajwa katika Mpangilio wa Kwanza.

(2) Serikali katika viwango vya kitaifa na kaunti ni tofauti na zinategemeana na Zitaendesha mahusiano yao ya uelewanaji kwa misingi ya mashauriano na ushirikiano.

(3) Asasi ya Serikali ya kitaifa itahakikisha ufikiaji wa huduma zake bora katika sehemu zote za Jamhuri kwa njia inayofaa na kulingana na hali ya huduma inayotakikana.