Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 188. Mipaka ya Kaunti

(1) Mipaka ya kaunti inaweza kubadilishwa kwa pendekezo tu–

  • (a) lililopendekezwa na Tume huru iliyobuniwa na bunge kwa lengo hilo; na
  • (b) liliyoidhinishwa na–
    • (i) Baraza la Kitaifa likiungwa mkono na wabunge wasiopungua thuluthi mbili wa bunge hilo; na
    • (ii) seneti ikiungwa mkono na angalau wawakilishi wa kaunti wasiopungua thuluthi mbili ya ujumbe wa kaunti.

(2) Mipaka ya kaunti inaweza kubadilishwa kwa kuzingatia–

  • (a) wingi wa watu na uongezekaji wao;
  • (b) miundomsingi na uhalisia wao;
  • (c) mshikamano wa kihistoria na misingi ya kitamaduni;
  • (d) gharama za usimamizi;
  • (e) maoni ya jamii zilizoathirika;
  • (f) malengo ya ugatuzi wa Serikali; na
  • (g) sifa za kijiografia.