Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 175. Kanuni za Serikali ya Ugatuzi

Serikali za kaunti zilizobuniwa chini ya Katiba hii zitazingatia kanuni zifuatazo–

  • (a) Serikali za kaunti zitazingatia misingi ya kidemokrasia na utengano wa mamlaka.
  • (b) Serikali za kaunti sharti ziwe na njia za kuaminika za kuzalisha mapato ili kuziwezesha kuendesha shughuli zao na kutoa huduma kwa njia bora; na
  • (c) isiyo zaidi ya theluthi mbili ya wanachama wawakilishi wa taasisi za umma katika Serikali za kaunti watakuwa wa jinsia moja.