Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

Kifungu 164. Mahakama ya Rufani

(1) Kutabuniwa Mahakama ya Rufaa, ambayo–

  • (a) itakuwa na idadi ya majaji ambao hawatapungua kumi na wawili kulingana na sheria za bunge; na
  • (b) inaundwa na kusimamiwa kulingana na ufafanuzi wa Sheria ya Bunge.

(2) Kutakuwa na Rais wa Mahakama ya Rufaa ambaye atachaguliwa na majaji wa mahakama ya Rufaa kutoka miongoni mwao.

(3) Mahakama ya Rufaa ina mamlaka ya kusikiza rufaa kutoka –

  • (a) Mahakama Kuu; na
  • (b) mahakama nyingine au mahakama maalum kulingana na Sheria ya Bunge.