Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

14. Utekelezaji wa Masharti Yanayohusu Serikali ya Ugatuzi

(1) Sheria zinazotajwa katika ibara ya 2 (3) (b) na ibara ya 15 zinaweza kutekelezwa iwapo Tume ya Utekelezaji wa Katiba hii na, iwapo pia Tume ya Ugavi wa Mapato imeundwa, zote mbili zimeshauriwa na mapendekezo yoyote ya Tume hizi yamekubaliwa na Bunge.

(2) Tume hizi zitapewa angalau siku thelathini kuchunguza sheria chini ya ibara ndogo ya (1).

(3) Ibara ndogo za (1) na (2) zitaisha wakati Tume ya Utekelezaji wa Katiba itakapovunjwa.