Ruka hadi Yaliyomo
AfroCave

11. Seneti

(1) Hadi pale ambapo Seneti ya kwanza itachaguliwa chini ya Katiba hii–

  • (a) majukumu ya Seneti yatatekelezwa na Baraza Kuu la Kitaifa; na
  • (b) jukumu lolote au mamlaka yoyote yanayohitajika kutekelezwa kwa pamoja na viwango vyote viwili vya Bunge au kimoja baada ya kingine, yatatekelezwa na Baraza Kuu la Kitaifa.

(2) Jukumu lolote au mamlaka ya Seneti, iwapo yatatekelezwa na Baraza Kuu la Kitaifa kabla ya tarehe inayotajwa katika ibara ndogo ya (1) , yatachukuliwa kuwa yalitekelezwa kikamilifu na Seneti.